8.3 C
New York
Thursday, February 26, 2026
Home ENTERTAINMENT Hivi Ndio Makanga Wa Nairobi UJibu Abiria

Hivi Ndio Makanga Wa Nairobi UJibu Abiria

Hivi Ndio Makanga Wa Nairobi UJibu Abiria

480

 

Kama hujawahikaa Nairobi,haya ndio majibu utapata kutoka kwa makanga wa huku ile siku utakuja

Njeri: Roysambu ni ngapi?

Makanga: Roysambu ni moja tu. Pengine kama Chinese wamejenga ingine.

Odhis: Hii gari haina watu bana.

Makanga: Kwani hao wawili wenye wamekaa hapo ndani ni ng’ombe?

Man: Wekeni nyimbo za Yesu tafadhali.

Makanga: Yesu bado hajatoa album. Akitoa tutaeka.

Mwikali: Excuse me conda…gari za Mwingi zinapandiwa wapi?

Makanga: Ziliacha kupandwa juu hazimei.

Man: Kwani mwisho wa gari ni wapi?

Makanga: Mwisho ni hapo penye number plate iko.

Karis: Ruaka ni how much?

Makanga: Sijaskia Ruaka ikiuzwa. But nikiskia nitakwambia.

Passenger: Shukisha dere.

Makanga: Tukishukisha dere utaendesha gari?

Johnny: Maze, hii gari iko na joto sana.

Makanga: Basi shuka upande fridge.

Total
0
Share